Hatua za kuomba kibali cha Kampuni binafsi ya ulinzi
1. Tengeneza akaunti ya kampuni tarajiwa kwenye mfumo kwa kujaza taarifa
zote zinazohitajika, ikiwemo majina matatu ya mkurugenzi mmojawapo na namba yake ya simu inayotumika.
Namba ya simu hiyo itatumika kama jina la mtumiaji (username) wakati wa kuingia kwenye mfumo.
Mtumiaji anatakiwa kuihifadhi vizuri namba hiyo pamoja na password yake, kwani vitatumika
kuingia kwenye mfumo katika hatua zinazofuata.
2. Baada ya kusajili/kuingia(login) utakutana na ukurasa ndani ya
ukurasa huo kuna kitufe(request permit) itakayo
kutaka ujaze taarifa kama itakavyoelezwa bila kusahau viamabata/nyaraka kama
maelezo hapo chini
3. Utatakiwa kuingia kwa mfumo mara kwa mara kujua mwenendo wa
maombi yako ya kibali
Vigezo vya kusajili kibali cha Kampuni binafsi ya ulinzi
1. Kampuni tarajiwa inatakiwa kuwa na wakurugenzi wasiopungua
wawili
2. Kampuni tarajiwa inatakiwa kuwa na Mkataba wa makubaliano
3. Wakurugenzi wote wawe na cheti cha hati ya tabia njema
4. Taarifa ya benki ya wakurugenzi
Nyaraka za kuambatisha
1. Mkataba wa makubaliano
2. Hati ya tabia njema
3. Taarifa ya benki
4. Wasifu wa wakurugenzi (cv)